Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Habari

KATIBU MKUU ABDULLA AKUTANA NA UJUMBE WA UBALOZI WA MAREKANI NCHINI


 Na Chedaiwe Msuya, WHMTH, Dodoma

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Bw. Mohammed Khamis Abdulla  amekutana na kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka ubalozi wa Marekani nchini ambao ni Mshauri wa Kisiasa na Uchumi  Bwn, Jonathan Howard pamoja na Mkuu wa Siasa Bw, Richard Allen ambapo wamezungumzia masuala mbalimbali kuhusu Teknolojia ya 5G, masuala ya Usalama wa Mtandao pamoja na Uhuru wa vyombo vya habari nchini.

Aidha,  wameipongeza Serikali kupitia Wizara hiyo kwa kukuza uhuru wa vyombo vya habari nchini na kuboresha Sheria inayosimamia huduma za habari nchini. 

Kikao hicho kiliudhuriwa na Kaimu Mkurugenzi wa Usalama wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mha. Stephen Mwita  Wangwe kimefanyika leo Septemba 7, 2023 katika ofisi za Wizara hiyo zilizopo mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma